Mkurugenzi
Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Felix
Ngamlagosi akizungumza na waandishi wa habari juu ya tuzo waliopata
Dubai katika udhibiti wa Nishati iliofanyika Ofisi za EWURA, leo
jijini Dar es Salaam, Kushoto ni Mhandisi wa Umeme EWURA, Anastas
Mbawalla.
Mkurugenzi
Mkuu wa EWURA, Felix Ngamlagosi akionyesha kitabu cha kinachofafanua
masuala ya mikataba katika sekta ya Nishati ambacho Mtaalam wa Mhandisi
wa Umeme, Anastas Mbawalla (kushoto)alishiriki katika kuandika kitabu
hicho.
Mhandisi
wa Umeme wa EWURA, Anastas Mbawalla akizungumza na waandishi wa habari
juu alivyoshiriki katika kuandika kitabu cha masuala ya mikataba ya
nishati iliofanyika leo katika ofisi za EWURA jijini Dar es Salaam,
Kulia ni Mkurugenzi Mkuu EWURA, Felix Ngamlagosi.(PICHA NA EMMANUEL
MASSAKA.GLOBU YA JAMII)
Na Chalila Kibuda,Globu ya
Jamii
MAMLAKA ya Udhibiti wa
Huduma za Nishati na Maji (EWURA),imeibuka mshindi wa mashindano ya Tuzo ya
Mdhibiti Bora wa mwaka wa Nishati 2015.
Akizungumza na waandishi wa
habari leo ofisini kwake jijini Dar es Salaam,Mkurugenzi Mkuu wa EWURA,Felix
Ngamlagosi amesema kuwa tuzo hiyo imetolewa Juni 8 mwaka huu kwenye uzinduzi
wa sherehe za 17 za Mkutano Mkuu wa Kila mwaka wa Nishati wa Afrika
uliofanyika Dubai.
Ngamlagosi amesema kuibuka
kwa EWURA katika Tuzo za Nishati inalenga kuwatambua wale wote
ambao wametoa mchango kwa maendeleo ya soko la nishati barani Afrika.
“Ushindi wa Tuzo ya
Udhibiti Bora wa mwaka wa nishati 2015 imetambua mchango wetu wa udhibiti
kutokana na huduma tunayotoa kwenye malengo ya kuboresha mazingira ya
uwekezaji katika sekta ya nishati kutokana na mahitaji”amesema
Ngamlagosi.
Amesema tuzo hiyo inaifanya
Tanzania sasa itambulike Kimataifa kwa kuwa na taasisi thabiti ya uhakika ya
udhibiti wa sekta nishati na maji ,ambalo ni jambo la muhimu kwa nchi kuendelea
kuimarisha imani ya wawekezaji ambayo inatakiwa sana katika kuvutia mitaji
binafsi kwenye sekta ya nishati.
Comments