Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimsikiliza Mwenyekiti wa Chama
cha Wafugaji Kanda ya Ziwa Bwa.Mugisha Murshad wakati alipokuwa akitoa
malalamiko ya wafugaji kwa ukatili wanaofanyiwa na askari wa wanyamapori
katika mapori mbalimbali ya hifadhi kanda ya ziwa.
Mwenyekiti huyo alisema kuwa wafugaji
wamekuwa wakifunga safari kwenda mkoani Dodoma kwa ajili ya kuonana na
mawaziri wahusika akiwemo, Waziri wa Maliasili na Utalii Lazaro
Nyalandu, Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi Dk.Titus Kamani ,
aliyekuwa Waziri wa Ardhi ,Nyumba na Maendeleo ya Makazi Profesa Anna
Tibaijuka na Waziri Mkuu Pinda.
Pia
alisema wamefanya vikao kati yao na wakuu wa wilaya za mkoa wa Kagera
pamoja na Mkurugenzi wa Wanyamapori lakini hakuna kilichoifanikiwa zaidi
ya kupewa tarehe ya kwamba ufumbuzi utapatikana.
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisoma taarifa ya vikao 17
vilivyofanyika kati ya Wafugaji hao (pichani) na viongozi mbalimbali
wa Serikali,kwa ajili ya kutafuta ufumbuzi wa mgogolo wao dhidi ya
Askari wanyama pori lakini hakuna maamuzi ama suluhisho
lililopatikana.Kinana amekutana na wafugaji
hao mapema leo katika kijiji cha Nyakanazi wilayani Biharamulo na kutoa
kero zao kwake juu ya manyanyaso wanayofanyiwa na askari wa
wanyamapori.
Alisema
kuna mambo mawili yamemsikitisha, moja watu kutumia mwavuli wa sheria
kufanya mambo yao binafsi kwani hakuna Serikali inayoweza kutumbukiza
ng'ombe kwenye shimo.
"Wizi
,rushwa ndicho kinachoonekana ndani yake, kwa maelezo yenu kuna baadhi
ya watendaji wameamua kuchukua sheria mkononi mwao.Wanachukua milioni 10
za mfugaji na kisha zinakwenda kwenye mifuko yao,"alisema.
Alisema
lazima akiri, Serikali nayo imelegea mno katika kuchukua maamuzi, kwani
amehesabu vikao ambavyo wafugaji wamekaa na viongozi wa ngazi
mbalimbali za juu serikali vipatavyo 17 lakini hakuna ufumbuzi na badala
yake ni maneno, maneno tu.
Alisema
kama wameshindwa kutatua matatizo ya watu ni vema wakaa kando maana
mishahara wanalipwa na marupurupu wanapewa lakini kushughukulikia
matatizo ya watu imekuwa ngumu.
"Watu
wameuawa, ng'ombe wamekufa, ng'ombe wameporwa.Hii haiwezekani na kwamba
matatizo yote yanayohusu wanyamapori wenye mamlaka ni Wizara ya
Maliasili na Utalii.
"Niombe
mambo mawili yafanyike, ng'ombe waliokamatwa warudishwe kwa wafugaji na
pili kesi zilizopo mahakamani zifutwe na wenye mamlaka ya kuzifuta ni
Serikali maana ndio waliofungua kesi,"alisema Kinana.
Baadhi
ya wafugaji wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana
hayupo pichani wakati alipokuwa akizungumza nao katika kijiji cha
Nyakanazi Wilayani Biharamulo mkoani Kagera.Kwa
mujibu wa wafugaji hao wameeleza kuwa wilaya zote zilizopo Mkoa wa
Kagera na hasa Wilaya ya Ngara , wafugaji wamekuwa wakipata mateso
makubwa pindi mifugo yao inapokamatwa kwenye pori la Kimisi ambapo
ng'ombe wamekuwa wakipigwa risasi na wengine kuingizwa kwenye shimo refu
lenye tope linalojulikana kwa jina la Gwantanamo.
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimsikiliza Mwenyekiti wa Chama
cha Wafugaji Kanda ya Ziwa Bwa.Mugisha Murshad wakati alipokuwa
akimuonyesha eneo linalotumika kuhifadhi mifugo yao mara inapokamatwa na
kuwa eneo hilo ni dogo na halina chakula cha mifugo wala maji jambo
ambalo hupelekea mifugo kufa kwa wingi.
Mmoja wa wafugaji akimuonesha Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana eneo ambalo mifugo inayokamatwa
hupelekwa hapo na kuwekwa kwa muda mrefu bila maji wala chakula na
matokeo yake mifugo hufa,iwapo mwenye mifugo hiyo hakwenda kuikomboa kwa
gharama itakayokuwa imetajwa,ambayo wafugaji hao wamekuwa
wakiilamimikia
Katibu
Mkuu wa CCM,Ndugu Kinana akioneshwa eneo ambalo mifugo ya Wafugaji
ilikuwa ikikusanywa eneo hilo na kuacha kwa muda mrefu bila chakula wala
maji na hatimae kupoteza uhai,jambo ambalo wafugaji hao wameona ni
kitendo cha uonevu na unyanyasaji mkubwa,kwani kwa kukamatwa mifugo yao
wamekuwa wakitozwa fedha nyingi kuikomboa mifugo yao,hivyo wameomba
Ndugu Kinana kusikiliza kilio chao cha mda mrefu.
Comments