KOMREDI KINANA ATUA KYERWA, AKAGUA SHAMBA BORA LA MIGOMBA, KAHAWA

 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana akitembelea shamba la mkulima bora wa migomba, Eurius Kishinju katika Kata ya Mabira, wilayani Kyerwa, mkoani Kagera. Kinana ambaye ameambatana na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho, Nape Nnauye wanaanza rasmi ziara mkoani Kagera, ya kuimarisha uhai wa chama, kukagua Utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi pamoja na kusikiliza kero za wananchi na kuzitafutia ufumbuzi

Kishinju ambaye ana shamba la migomba heka 3 mchanganyiko na kahawa, kwa mwezi huuza mikungu 43 kwa mwezi ambapo kila mkungu huuza kwa sh. 10,000, hivyo kujipatia kitita cha sh. 430,000, pia hvuna magunia 25 ya kahawa, ambapo sehemu ya mapoato hayo amejengea nyumba ya kisasa na kusomesha watoto wake wawili katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Chuo Kikuu cha Dodoma.PICHA ZOTE NA RICHARD MWAIKENDA;KAMANDA WA MATUKIO BLOG
 Komredi Kinana akioneshwa zao la kahawa alipotembelea shamba hilo
 Komredi Kinana akikagua shmba bora la migomba na kahawa katika Kata ya Mabira, linalomilikiwa na mkulima Kishinju
 Wananchi wa Kata ya Nkwenda wakimpigia makofi Katibu Mkuu wa CCM, Komredi Kinana alipokuwa akihutubia katika Kijiji cha Nkwenda, wilayani Kyerwa, ambapo aliahidi kufikisha kilio cha bei ndogo ya kahawa katika vikao vya ngazi ya juu na hasa Kamati Kuu ya CCM Julai mwaka huu, ili wakulima wa zao hilo waruhusiwe kuuza watakako kwenye bei kubwa.
 Katibuwa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye akihutubia katika mkutano wa hadhara katika viwanja vya Shule ya Sekondari ya Kikukuru, Katika Kata ya Mabira, wilayani Kyerwa. Mabira Kikukuru
 Wananchi wakishangilia wakati wa mkutano huo
 Komredi Kinana akihutubia katika mkutano wa hadhara katika Kata ya Mabira, wilayani Kyerwa, mkoani Kagera
Wananchi wakimsalimia Katibu Mkuu wa CCM, Komredi Kinana alipokwenda kukagua  Zahanati yaKijiji cha Kigorogoro wilayani Kyerwa, Kagera.
 Wananchi wakiwa na furaha wakati wa kumlaki Komredi Kinana katika Kijiji cha Kigorogoro, wilayani Kyerwa
 Komredi Kinana akihutubia alipokagua maendeleo ya ujenzi wa Soko la Kimataifa la Murongom wilayani Kyerwa, ambao hivi sasa umesimama.Soko hilo lipo mpakani mwa Tanzania na Uganda.
 Wananchi bwa Kata ya Kaisho, Kijiji cha Kibingo wakishangilia walipokuwa wakimlaki Katibu Mkuu wa CCM, Komredi Kinana ambaye alifanya ziara katika eneo hilo kuzindua mradi wa maji na kuhutubuia wananchi.

 Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye, ,AKIWA AMESIMAMA KWENYE GARI AKIANGALIA MWENENDO WA MKUTANO WA HADHARA KATIKA KIJIJI CHA KIBINGO, WILAYANI KYERWA.
 Komredi Kinana akihutubia mkutano wa hadhara katika Kijiji cha Kibingo, Kata ya Murongo.
 Wananchi wakiwa na hamu ya kumsalimia alipowasili katika Mji wa Isingiro,Makao Makuu ya Wilaya ya Kyerwa, mkoani Kagera.
 Komredi Kinana akisalimiana na wananchi katika Mji wa Isingiro, wilayani Kyerwa, Kagera.
 Ni furaha iliyoje kwa wakazi wa Mji wa Isingiro walipokuwa wakimlaki, Komredi Kinana
 Mbunge wa Jimbo la Kyerwa, Kategile akielezea miradi mbalimbali aliyoitekeleza jimbo humo ikiwa ni utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi wakati wa mkutano huo wa hadhara
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Napoe Nnauye akihutubia katika mkutano huo.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI