Waombolezaji wakiwa wamebeba jeneza
lenye mwili wa Mhariri wa Kampuni ya Mwanahalisi, Edson Kamukara wakati
ulipowasili viwanja vya Leaders Club Dar es Salaam leo asubuhi, kwa
ajili ya kuagwa. Kamukara alifariki dunia juzi na mazishi yake
yanatarajia kufanyika nyumbani kwao Muleba mkoani Kagera.
Mwenyekiti wa Umoja wa Wamiliki wa
Vyombo vya Habari Tanzania (MOAT), Regnald Mengi (katikati), akiwa na
Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk.Wilibrod
Slaa kwenye uagaji wa mwili wa Edson Kamukara. Kulia ni Mbunge wa Bukoba
mjini, Khamis Kagasheki.
Mmoja wa waandishi wa habari akiwa amepoteza fahamu wakati wa kuaga mwili huo.
Wanahabari na waombolezaji wengine
wakiwa wamejipanga foleni wakati wa utoaji wa heshima za mwisho kwa
mwili wa marehemu Edson Kamukara.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Mwanahalisi,
Said Kubenea (katikati), akisaidiwa baada ya kuishiwa nguvu wakati
akitoa heshima za mwisho kwa marehemu
Wanahabari ni huzuni na vilio
Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na
Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe akisalimiana na Mbunge wa Bukoba
mjini, Balozi Khamis Kagasheki wakati wa kuuaga mwili wa Edoson
Kamukara.
Wanafamilia ya marehemu wakiwa kwenye shughuli hiyo
Sehemu ya umati wa watu katika shughuli hiyo.
Mwakilishi wa wanafunzi waliosoma na
marehemu Shule ya Sekondari ya Majengo, Joachim Mushi akizungumza kabla
ya kutoa rambirambi yao ya sh.500,000.
Viongozi wa serikali na vyama vya siasa wakiwa kwenye shughuli hiyo. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Paul Makonda.
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul
Makonda akizungumza katika uagaji wa mwili wa marehemu ambapo alipigania
waajiri wa vyombo vya habari kutoa mikataba ya ajira kwa wanahabari.
Mwenyekiti
wa Umoja wa Wamiliki wa Vyombo vya Habari Tanzania (MOAT), Regnald
Mengi akimfariji Mkurugenzi wa Kampuni ya Mwanahalisi, Said Kubenea
alikuwa akifanyakazi marehemu Edson Kamukara.
Ni vilio tu kwa wanahabari.
Shughuli ya uagaji ikiendelea.
Dada ya marehemu Edson Kamukara akitoa heshima za mwisho.(PICHA NA KHAMISI MUSSA)
Comments