MCC, Makampuni 10 ya Kimarekani yamaliza ziara ya kuangalia fursa za biashara na uwekezaji nchini Tanzania

Makamu wa Rais wa Shirika la Changamoto za Milenia (MCC) Kamran Khan ( wa pili kulia)  akifafanua jambo wakati wa mkutano kati ya Waziri Mkuu wa Tanzania Mizengo Pinda (katikati) na wawakilishi wa makampuni 10 ya Kimarekani, walipomtembelea ofisini kwake jijini Dar es Salaam hivi karibuni. Bw. Khan aliongoza ziara ya wawakilishi hao wa makampuni ya kimarekani, Wizara ya Biashara ya Marekani na MCC ili kuangalia fursa za uwekezaji katika sekta ya nishati nchini Tanzania.
====  =======  =======
Shirika la Changamoto za Milenia (MCC), Wizara ya Biashara ya Marekani na  makampuni 10 ya Kimarekani hivi leo wamemaliza kwa mafanikio mkubwa ziara yao ya kuangalia fursa za biashara na uwekezaji katika sekta ya nishati katika nchi za Tanzania.
Ziara hii ya kwanza na ya aina yake katika historia ya miaka 11 ya MCC, ililenga kukuza mauzo ya nje ya bidhaa zinazozalishwa na makampuni ya Kimarekani na kuongeza uwepo wa makampuni hayo barani Afrika kwa kutambulisha kwayo fursa mbalimbali zilizopo za uwekezaji katika sekta ya nishati. 

Aidha, ziara hii ililenga kuchangia katika kufikia malengo ya Mpango Maalumu wa Serikali ya Marekani wa Kusaidia Maendeleo ya Sekta ya Nishati barani Afrika uitwao “Power Africa” unaolenga kuongeza mara mbili kiwango cha upatikanaji wa umeme katika nchi za Afrika zilizo kusini mwa jangwa la Sahara. 
Makampuni haya yalipata fursa ya kukutana na viongozi waandamizi wa Serikali ya Tanzania ikiwa ni pamoja na Waziri Mkuu Mizengo Pinda, pamoja na wawakilishi wa sekta binafsi ya Tanzania na asasi zisizo za kiserikali
Aidha, wajumbe wa ziara hii walikutana na Balozi wa Marekani nchini Tanzania Mark Childress na Naibu Waziri wa Nishati wa Marekani Christopher A Smith. Aidha wajumbe walipata maelezo kuhusu fursa za uwekezaji katika sekta ya nishati nchini Tanzania kutoka kwa wawakilishi wa MCC, Wizara ya Biashara ya marekani, Shirika la Marekani la Ushirikiano wa Kimataifa (USAID) na Chama cha Wafanyabiashara wa Kimarekani nchini Tanzania.
“Sekta ya nishati ya Tanzania ipo tayari kwa wawekezaji wan je, tungependa makampuni ya Kimarekani yajionee yenyewe na kusikia kutoka kwa viongozi waandamizi wa nchi hii kuhusu fursa zilizomo nchini humu,” alisema Kamran Khan, Makamu wa Rais wa Idara ya Usimamizi

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI