NEC YATISHIA KUSITISHA ZOEZI LA UANDIKISHAJI ARUSHA NA KILIMANJARO


Tume ya taifa ya uchaguzi nchini NEC imetishia kusitisha zoezi la uandikishaji wananchi katika daftari la kudumu la wapiga kura katika miji ya Arusha na Kilimanjaro endapo viongozi wa kisiasa wataendelea kuingilia mchakato huo na kuwa vyanzo vya vurugu katika vituo vya kuandikishia.
Ni mwenyekiti wa tume ya taifa ya uchaguzi NEC Jaji Mstaafu Damiani Lubuva akielezea masikitiko ya tume kufuatilia kile alichokiita ni kuingiliwa kwa maafisa wa tume katika kazi zao za uandikishaji katika miji ya Arusha na Kilimanjaro jambao lililopelekea kuzuka kwa vurugu katika baadhi ya vituo ndani ya mikoa hiyo.
Jaji Damian amesema katika mahojiano yake maalum na ITV jijini Dar es Salaam, kuwa tangu kaunza kwa zoezi la uandikishaji kumekuwa na changamoto kadha ambazo hata hivyo tume ilijitahidi kuzitatua lakini kwa hali ya Arusha na Kilimanjaro huenda tume ikalazimika kufanya maamuzi magumu.
Amesisitiza kuwa ni vema viongozi wa kisiasa wakahakikisha wanakuwa mstari wa mbele katika kufanikisha zoezi hilo ambalo kwasasa limekwisha kukamilika kwa zaidi ya asilimia 85, ambapo pia amesisitiza kuwa kwa hali ilivyo hivi sasa uchaguzi utafanyika kama ulivyopangwa kwani kila kitu kiko katika hali ya ukamilifu.
Katika mahojaino hayo pia jaji Lubuva amezungumzia suala la uandikishwaji kwa upande wa Zanzibar ambapo anasema zoezi hilo linatarajia kuanza muda wowote akuanzia sasa huku akisisitiza utulivu wakati wa zoezi hilo.

- See more at: http://tanzaniagazeti.blogspot.com/2015/06/nec-yatishia-kusitisha-zoezi-la.html#sthash.pyBFOKVT.dpuf

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.