RAIS KIKWETE AANZA ZIARA YA NCHI TATU ULAYA
THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
Telephone: 255-22-2114512, 2116898
E-mail: ikulucommpress@googlemail.com
Website : www.ikulu.go.tz
Fax: 255-22-2113425 |
PRESIDENT’S OFFICE,
STATE HOUSE,
1 BARACK OBAMA ROAD,
11400 DAR ES SALAAM.
Tanzania.
|
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais Kikwete aanza ziara ya nchi tatu Ulaya.
Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete
leo, Jumatatu, Juni Mosi, 2015 ameanza ziara rasmi ya wiki moja katika
nchi tatu za Ulaya kwa mwaliko wa viongozi wa nchi hizo.
Rais
Kikwete ambaye aliondoka nchini usiku wa jana, Jumapili, Mei 31, 2013
baada ya kumaliza kuendesha Mkutano wa Wakuu wa Nchi Wanachama wa Jumuia
ya Afrika Mashariki (EAC) kuhusu Burundi ameanzia ziara yake katika
Finland ambako atakaa kwa siku tatu.
Baadaye, Rais Kikwete atatembelea nchi za Sweden na Uholanzi kabla ya kurejea nyumbani.
Katika
Finland, Rais Kikwete miongoni mwa mambo mengine kesho Jumanne, Juni 2,
2015, atafanya mazungumzo rasmi ya Kiserikali na Rais wa nchi hiyo na
baadaye atatembelea Bunge la nchi hiyo ambako atafanya mazungumzo na
Wabunge.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.
1 Juni, 2015
Comments