SERIKALI KUTUMIA TEKNOLOJIA YA JENI KATIKA KUENDELEZA

 
2
Naibu Waziri, Wizara ya Ushirikiano wa Afika Mashariki, Mhe. Dkt. Abdullah Saadala, akijibu swali Bungeni Dodoma leo.3
Naibu Waziri, Wizara ya Kazi na Ajira, Mhe. Makongoro Nyerere (Mb) akijibu swali katika kipindi cha maswali na majibu leo Bungeni Dododma.
4
Mbunge wa Viti Maalum Mhe. Martha Mlata (aliyesimama) akitoa hoja Bungeni Dodoma leo, akitaka Serikali itoe msimamo kuhusu mgogoro wa Ashanti na Wazawa katika migodi ya Mkoani singida.
5
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Utawala Bora, Mhe. George Mkuchika, akijibu swali Bungeni Dodoma leo, la Mhe. Fakharia Shomar Khamis (Viti maalumu), aliyetaka kujua idadi ya viongozi waliofikishwa katika Tume ya Maadili kutokana na makosa ya ukiukwaji wa maadili.
6
Mbunge wa Vunjo, Mhe. Augustino Lyatonga Mrema (aliyesimama) akisalimiana na Mhe. Lekule Leizer (Mb), Loliondo, wakati akiingia Bungeni Dodoma leo

7
Mbunge wa Viti Maalumu, Mhe. Esther Bulaya, akiuliza swali la nyongeza kuhusu matumizi ya vipodozi vyenye madhara kwa afya ya binadamu Bungeni Dodoma leo, katika kipindi cha maswali na majibu.
8
Naibu Waziri, Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Mhe. Dkt. Stephen Kebwe (Mb) akijibu swali Bungeni Dodoma leo, la Mhe. Muhammad Ibrahim Sanya (Mji Mkongwe) aliyetaka kujua kuhusu jitihada za serikali katika kudhibiti kuingizwa kwa bidhaa za vipodozi vyenye madhara kwa matumizi ya binadamu.
9
Naibu Waziri, wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na watoto Mhe. Pindi Chana (Mb) akijibu swali leo Bungeni Dodoma, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika kuhusu mpango wa Serikali kutumia teknolojia ya jeni katika kuboresha mbegu za mazao.
10
Mbunge wa Viti maalum, Mhe. Ana Abdallah akibadirishana mawazo na Mhe. Laidiana Mung’ong’o nje ya ukumbi wa Bunge, leo Dodoma.
11
Mbunge wa Kawe, Mhe. Halima Mdee (CHADEMA) kushoto, akiteta na Mbunge mwenzake, Mhe. Cecilia Paresso (CHADEMA) mara baada ya kikao cha Bunge leo, Dodoma.
Na. Georgina Misama…Maelezo…Dodoma
……………………………………………………………………
Serikali imeandaa mpango wa kuendeleza mazao ya pamba, muhogo, mahindi na migomba kwa kutumia utaalam wa uhandisi jeni.
Hayo yameelezwa bungeni leo na Naibu Waziri, Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Mhe Pindi Chana wakati akijibu swali kwa niaba ya Waziri wa Kilimo Chakula na Ushirika, lilioulizwa na Mhe. Dkt. Henry Daffa Shekifu (Mb) Lushoto, aliyetaka kujua serikali ina mpango gani wa kuanzisha kilimo cha mazao kwa kutumia utaalam wa jeni.
Mhe. Chana amesema kuwa, chini ya mpango huo, Serikali imeimarisha uwezo wa utafiti, Miundombinu ya maabara na mashamba maalum kwa aajili ya kufanya utafiti.
Amesema hata hivyo, utekelezaji wa mipango hiyo umeathiriwa na uwepo wa kipengele cha dhima kali katika kanuni za kusimamaia matumizi salama ya bioteknolojia ambacho kinalenga kuwajibisha utafiti wa mazao ya jeni endapo madhara yoyoyte yatatokea.
Amesema hata hivyo serikali kwa kuzingatia umuhimu wa manufaa ya uhandisi jeni katika kuleta mapinduzi ya kilimo, umefanya marekebisho ya kanuni hizo kwa kuondoa dhima kali katika utafiti ili kuwezesha kufanyika katika mazao ya kilimo.
Mhe. Chana amesema kuwa wataalam wetu wamejifunza utaalam huo na wanao uwezo wa kuitumia teknolojia hiyo, ambapo kwa mfano katika utafiti wa maabara, kwa kutumia uhandisi jeni, wameweza kugundua jeni katika muhogo ambazo zina ukinzani wa magonjwa ya batobato na michirizi kahawia ya muhogo.
Amesema kuwa, serikali itaendelea kuwaelimisha wananchi, kuhusu manufaa ya teknolojia ya uhandisi jeni katika kuleta maendeleo ya kilimo.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.