Mgeni
rasmi wa hafla ya uzinduzi wa Programu ya Kukuza Ajira zenye Staha kwa
Vijana wa mkoa wa Dar es Salaam (YEID) amabaye pia ni Afisa Vijana
kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bw. Godfrey Nyaisa
(wapili kulia) akiwa katika picha yenye bango linalohamasisha vijana
kujiandikisha katika Daftari la kudumu la Wapiga Kura juzi jijini Dar es
Salaam.
Afisa
Vijana kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Gofrey
Nyaisa akizungunza na vijana wa mkoa wa Dar es Salaam wakati wa hafla ya
uzinduzio wa Programu ya Kukuza ajira zenye Staha kwa vijana wa mkoa
huo (YEID) juzi jijini hapa.Program hiyo inatekelezwa kwa ushirikiano
wa asasi za kirai za Open Mind Tanzania (OMT), Tanzania Youth Vision
Association (TYVA) na Youth for Africa (YOA).
Mratibu
wa Programu ya kukuza Ajira zenye Staha Dar es Salaam, kupitia Elimu ya
Biashara na Maendeleo ya Ujasiriamali Bw. Dominic Ndunguru akizungumza
na washiriki wa hafla ya uzinduzi wa Programu hiyo juzi jijini Dar es
Salaam. Programu hii inaendeshwa kwa ubia wa asasi za kiraia za Tanzania
Youth Vission Associataion (TYVA), Open Mind Tanzania (OMT) na Youth
For Africa (YOA).
:
Baadhi ya Vijana waliohudhuria hafla ya uzinduzi wa Programu ya Kukuza
Ajira zenye Staha Dar es Salaam wakiangalia baadhi ya huduma zitolewazoi
na asasi mbalimbali za Vijana walipofanya maonyesho yaliyoenda sambamba
na uzinduzi huo juzi katika viwanja vya Don Bosco Youth Center jijini
Dar es Salaam
Afisa
Vijana kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Gofrey
Nyaisa akikabidhi Cheti kwa mmoja wa wahitimu wa mafunzo ya Maendeleo ya
Biashara na Ujasiriamali Bi. Lilian Daniel wakati wa hafla ya uzinduzi
wa Programu ya Kukuza ajira zenye Staha kwa vijana wa mkoa wa Dar es
Salaam (YEID) juzi jijini hapa. Jumla ya vijana 105 kutoka katika
masnispaa za Ilala, Temeke na Kinondoni walipata mafunzo hayo
yanayoendeshwa na asasi za kiraia za Tanzania Youth Vission Associataion
(TYVA), Open Mind Tanzania (OMT) na Youth For Africa (YOA).
…………………………………………………………………………..
Na: Frank Shija, WHVUM
Serikali
imeahidi kuendelea kushirikiana na wadau wote walio na dhamira na
mueleko wa dhati katika kuhakikisha tunatatua changamoto za ajira kwa
Vijana nchini.
Kauli
hiyo imetolewa juzi jijini Dar es Salaam na Afisa Vijana kutoka Wizara
ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bw. Godfrey Nyaisa alipokuwa
mgeni rasmi wakati wa hafla ya uzinduzi wa Programu ya Kukuza Ajira
zenye Staha kwa Vijana wa mkoa wa Dar es Salaam (YEID).
Nyaisa
amesema kuwa Serikali imeendelea kuchukulia kwa uzito stahiki suala la
ajira kwa vijana ikiwemo kuanzisha program mbalimbali kwa lengo la
kumsaidia kijana aweze kujikwamua kiuchumi na kuondokana na changamoto
za ajira zinamzomkabili kijana.
Aliongeza
kuwa mpaka sasa Serikali imekwisha tekeleza mambo mbalimbali ikiwemo
kuwapa mafunzo vijana ambapo jumla ya vijana 1550 wamekwisha pati wa
mafunzo ya ujasiriamali na stadi za maisha kupitia mfuko wa maendeleo ya
vijana na kusongeza kuwa mafunzo hayo ni endelevu.
“Niseme
tu Serikali itaendelea kushirikiana na wadau wote wenye dhamira ya
dhati ya kumletea maendeleo kijana ili aweze kujikwamu” Alisema Nyaisa.
Awali
akimkaribisha mgeni rasmi Mratibu mwenza wa Programu ya Kukuza Ajira
zenye Staha kwa Vijana wa mkoa wa Dar es Salaam (YEID) kupitia Elimu ya
Biashara na Maendeleo ya Ujasiriamali Bw. Dominic Ndunguru amesema kuwa
imekuwa ni faraja kwao kupata ushirikiano kama huo kutoka Serikali hii
na kuongeza kuwa hii ni dalili njema kwao kuwa Programu hiyo itakuwa na
matokeo chanya na kwa muda mfupi.
Ndunguru
alisema kuwa Programu hiyo ya Kukuza Ajira zenye Staha ilianza kama
majaribio tokea mwaka 2014 na kuonyesha mafanikio hivyo ni furaha kwao
kuone leo (juzi) inazinduliwa rasmi ikiwa tayari imeleta matunda kwa
vijana.
Aliongeza
kuwa kupitia Programu hiyo vijana watapata fursa ya kupata bure elimu
ya Ujasiriamali na Maendeleo ya Biashara, taarifa mbalimbali zinzaohusu
vijana, na fursa ya kushiriki mafunzo ya stadi za maisha na matumizi ya
Tehama.
Kwa
upande wake mmoja wa Vijana walionufaika na Programu hiyo Bi. Lilian
Daniel kutoka Manispaa ya Temeke ameelezea kufurahishwa kwake na ujio wa
Programu hii kwa kuwa imemfanya apate ujasiri wa kuthubutu kufanya
maamuzi katika masuala mbalimbali.
Ameongeza
kuwa Programu hiyo itasaidia sana kwa kuwa inatoa fursa ya kupata elimu
ya bure hivyo kwa wasiokuwa na uwezo wa kuendelea na elimu ya Sekondari
na ata vyuo wanayo fursa ya kuelimika kupitia Progra hii iliyozinduliwa
rasmi leo. Alisema Lilian
Programu ya Kukuza Ajira zenye Staha kwa mkoa wa Dar es Salaam ambayo kwa kiingeraza inaitwaYouth Employability Initiative in Dar es Salaam (YEID)
inatekelezwa kwa ubia baina ya asasi tatu za kirai ambazo ni Tanzania
Youth Vision Association (TYVA), Open Mind Tanzania na Youth for Africa
(YOA) katika Manispa za Ilala, Temeke na Kindoni jijini Dar es Salaam
Comments