Timu
ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) inayodhaminiwa na bia ya Kilimanjaro
Premium Lager, leo imepoteza mchezo wake wa kwanza kuwania kufuzu kwa
fainali za AFCON mwaka 2017 baada ya kufungwa kwa mabao 3 - 0 na wenyeji
Misri.
Taifa
Stars ilicheza vizuri kipindi cha kwanza na hasa sehemu ya ulinzi
ilifanya kazi ya ziada kuokoa mashambulizi ya washambuliaji wa timu ya
Misri, na kupelekea kwenda mapumziko -0 - 0.
Kipindi
cha pili Misri walifanya mabadiliko yaliyowapelekea kupata mabao hayo 3
ndani ya dakika 10, kupitia kwa Ramy Rabia(60), Basem Morsy(64) na
Mohamed Salah (69).
Stars
ilifanya mabadiliko ya kuwaingiza Frank Domayo, Saimon Msuva na Salim
Mbdonde na kufanya shambulizi kadhaa langoni kwa Misri lakini
mashambulzi hayo yaliokolewa na walinzi wa timu ya Misri.
Mara
baada ya mchezo huo, Taifa Stars inaondoka leo Alexandria kuelekea
Cairo ambapo itaondoka na shirika la ndege la Ethiopia saa 8 usiku na
kufika jijini Dar es salaam jumanne saa 7 mchana.
Tanzania:
Deogratias Munish, Shomari Kapombe, Oscar Joshua, Aggrey Morris/Salim
Mbonde, Nadir Haroub, Erasto Nyoni, Jonas Mkude, Mwinyi Kazimoto/Saimon
Msuva, Thomas Ulimwengu, Mbwana Samata, Amri Kiemba/Frank Domayo.
Misri:
Ahmed El Shenawy, Ahmed Hegazy, Ramy Rabea, Mohamed Abd Elshafy, Hazem
Emam, Mohamed Elneny, Ibrahim Salah, Mahmoud Abd Elmonem/Ramadan Soffiy,
Mohamed Salah/Mostafa Ftahy, Doly Elgabay/Basem Morsy, Ahmed Hassan
Meky.
TIMU
ya taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' jana usiku imechapwa magoli 3-0
dhidi ya Misri katika mechi ya kuwania kufuzu fainali za mataifa ya
Afrika (Afcon 2017) iliyochezwa mjini Alexandria.
Magoli
ya Misri yalifungwa dakika ya 61' na Rami Rabia, dakika ya 65' na Basem
Morsi na msumari wa mwisho ukatiwa kimiani dakika ya Mohamed Salah
dakika ya 70'.
Stars walijitahidi kuwazuia Misri kwa dakika 60', lakini walipoteza mwelekeo ndani ya dakika 10' tu na kupigwa magoli matatu.
Kipigo
hicho kinaiingiza Stars kwenye orodha ya nchi nyingine zilizopokea
kichapo jana ambapo imeshika namba mbili kwa kufungwa magoli mengi
katika mechi za jana jumapili.
Mauritius ndio vinara wa kuburuzwa jumapili ya jana kwani walifungwa 7-1 na timu bora ya Ghana.
Comments