Waziri wa
Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Uratibu na Bunge Mhe. Jenista Mhagama
(mwenye nguo nyekundu) akimfariji Mwenyekiti wa Bunge Bi. Lediana
Mng’ong’o mara baada ya bunge kuahirishwa kufuatia kifo cha aliyekuwa
Mbunge wa Ukonga Bi. Eugen Mwaiposa. Kulia ni Waziri wa Nchi Ofisi ya
Rais Utawala Bora Bi. Mary Nagu na kushoto ni wabunge James Mbatia na
Goodluck Ole Medeye.
Naibu
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Anjela Kairuki
(kushoto) akitoka nje ya ukumbi wa bunge akiwa ameambatana na wabunge
Bi. Mary Mwanjelwa na Rita Kabati baada ya bunge hilo kuahirishwa
kufuatia kifo cha Mbunge wa Ukonga Bi. Eugen Mwaiposa.
Baadhi ya
wabunge wakiwa kwenye hali ya simanzi baada ya kutangazwa kifo cha
aliyekuwa mbunge wa Ukonga Bi. Eugen Mwaiposa kilichotokea usiku wa
kuamkia leo nyumbani kwake mjini Dodoma.
Comments