WADAU WA MODEWJI BLOG WAJUMUIKA KUSHEREHEKEA MIAKA 7 YA MTANDAO HUO NDANI YA VIWANJA VYA SABA SABA

IMG_5219
Mdau wa modewjiblog, Ray the hustler (kushoto) aliyeambatana ndugu zake kutembelea banda la Modewjiblog katika picha ya pamoja na Mwandishi wa habari mwandamizi wa mtandao wa Modewjiblog, Andrew Chale.
Na Modewjiblog team
Shamra shamra za miaka Saba za mtandao wa habari nchini wa Modewji blog tayari zimeanza kurindima ndani ya banda la MeTL Group lililopo kwenye maonyesho ya 39 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar-es-salaam yaliyoanza jana kwenye mabanda ya SabaSaba katika viwanja vya Mwalimu J.K. Nyerere, barabara ya Kilwa, jijini Dar es Salaam.
Wadau mbalimbali wanaoperuzi mtandao wa modewji blog wamekuwa wakimiminika kujionea utendaji wa kazi zinazofanywa na mtandao huu pamoja na kupata picha za pamoja ikiwemo ‘selfie’ ambazo zinakuwa zinarushwa moja kwa moja katika blog na mitandao mingine ya kijamii ikiwemo facebook, twitter na Instagram.
Pia wadu na watu mbalimbali wanakaribishwa kutoa maoni yao namna ya kuboresha zaidi huduma zetu. 
Hata hivyo, kwa mujibu wa Meneja mwendeshaji Mkuu wa modewji blog, Zainul Mzige aliweza kutoa punguzo maalum la hofa kwa watu mbalimbali kujitokeza kutangaza na mo dewji blog katika msimu huu wa maonyesho ya Saba saba.
Punguzo hilo ni maalum na litadumu kwa muda wote wa kipindi cha Saba Saba pekee.
Kwa matangazo na maelezo zaidi wasiliana nasi kwa barua pepe : info@modewjiblog.com au zainul@modewjiblog.com
DSC_0582
Afisa Masoko wa taasisi ya Miradi na Maendeleo ya Miundombinu iliyochini ya Wizara ya Fedha, (UTT-PID), Kilave Atenaka (katikati) pamoja na Afisa kutoka taasisi hiyo Beatrice Ngode waki-show love na T-shirts za modewjiblog walizokabidhiwa walipotembelea banda la modewjiblog na kujionea shughuli mbalimbali za utendaji kazi wa mtandao huo katika shamra shamra za kusheherekea miaka 7 mtandao huo tangu ulipoanzishwa. Kulia ni Mwandishi wa mwandamizi wa modewjiblog, Andrew Chale.
IMG_5195
Mdau wa Modewjiblog, Bw. Geofrey Tupper (kushoto) akipokea fulana kutoka kwa Mwandishi mwandamizi wa mtandao wa modewjiblog, Andrew Chale mara baada ya kutembelea banda lao katika maonyesho ya saba saba yaliyoanza kutimua vumbi jana jijini Dar es Salaam.
IMG_5204
Mbunifu wa mavazi nchini Ally Rehmtulah (wa pili kushoto) akipata picha ya kumbukumbu na team ya modewjiblog pamoja na mdau wa kampuni ya vifaa vya ki-elektoniki ya LG katika aliptembelea letu katika banda la maonyesho ya saba saba yalioanza kutimu vumbi jana jijini Dar es Salaam.
DSC_0579
Maafisa wa tasisi ya UTT-PID waki-show love na kofia pamoja na T-shirts za modewjiblog mara baada ta kutembelea banda hilo kwenye maonyesho ya saba saba.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.