Wananchi walivyotembelea mradi wa viwanja Vikuruti

Baadhi ya wananchi wakiangalia ramani katika mradi wa viwanja unaoendeshwa na Taasisi ya Kifedha ya Bayport Financial Services, katika eneo la Vikuruti, wilayani Kibaha, mkoani Pwani mwishoni mwa wiki na kusimamiwa na Meneja Mauzo wa Taasisi hiyo Nasra Sudi. Picha zote na Mpigapicha Wetu.
Wananchi waliokwenda kuonyeshwa viwanja hivyo wakipata somo la mradi huo wa vianja vya Vikuruti unaoendeshwa na Taasisi ya Bayport Financial Services.
Wananchi hawa wakiangalia kwa makini ramani ya viwanja vya Vikuruti, vinavyoratibiwa na Taasisi ya Kifedha ya Bayport Financial Services, mwishoni mwa wiki. Zoezi la viwanja hivyo kwa watumishi wa umma, wafanyakazi wa kampuni binafsi na wajasiriamali linaendelea hadi Juni 30 mwaka huu, ambapo kila Mtanzania anaweza kupata kiwanja hicho kwa fedha taslimu au kwa mkopo. Thamani ya viwanja hivyo inaanzia Sh 1,400,000 na kuendelea.
Afisa Mauzo wa Bayport Financial Services, Catherine Tesha, akitoa maelekezo kwa baadhi ya wananchi waliokwenda Vikuruti, wilayani Kibaha, mkoani Pwani kujipatia fursa ya viwanja vinavyoratibiwa na Taasisi ya Kifedha ya Bayport Financial Services, mwishoni mwa wiki. Zoezi la viwanja hivyo kwa watumishi wa umma, wafanyakazi wa kampuni binafsi na wajasiriamali linaendelea hadi Juni 30 mwaka huu, ambapo kila Mtanzania anaweza kupata kiwanja hicho kwa fedha taslimu au kwa mkopo. Thamani ya viwanja hivyo inaanzia Sh 1,400,000 na kuendelea.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI