Balozi
wa Ireland nchini Tanzania Bi Fionnuala Gilsenan akisaini kitabu cha
wageni alipomtembelea Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
William Lukuvi (kushoto) ofisini kwake leo jijini Dar es salam.
Waziri
wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi akiongea na
mgeni wake Balozi wa Ireland nchini Tanzania Bi Fionnuala Gilsenan
(kulia) leo jijini Dar es salam. Kushoto ni Kamishna wa Ardhi nchini
Dkt. Moses Kusiluka.
Balozi
wa Ireland nchini Tanzania Bi Fionnuala Gilsenan akisisitiza jambo
wakati alipomtembelea Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
William Lukuvi (kushoto) ofisini kwake leo jijini Dar es salam.
Balozi wa Ireland nchini
Tanzania Bi Fionnuala Gilsenan akiwaonesha Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo
ya Makazi William Lukuvi (katikati) na Kamishna wa Ardhi nchini Dkt. Moses
Kusiluka (wa kwanza kushoto) baadhi ya picha na michoro inayoonesha namna bora
ya matumizi ya ardhi kulingana na matumizi husika ikiwemo mipango miji na
vijiji.(picha na Eleuteri Mangi-MAELEZO)
Na
EleuteriMangi-MAELEZO
Serikali
inadhamira yadhati kuboresha huduma ya ardhi nakuipeleka karibu na wananchi kwa
wakati ili iwe na tija kwa maendeleo endelevu.
Hayo yamebainishwa
na Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi alipokuwa akiongea
na Balozi wa Ireland nchini Tanzania Bi
Fionnuala Gilsenan leo jijini Dra es salam.
Akifafanua
kuhusu namna huduma hiyo itakavyopelekwa karibu na wananchi, Waziri Lukuvi amesemakuwa
wizara yake imeanzisha kanda nane ili kusogeza huduma za ardhi karibu na wananchi
badala ya hali ilivyokuwa zamani ambapo huduma hizi zilitolewa makao makuu ya wizara
hiyo tu yaliyopo jijini Dar es salaam.
“Ili
kutoa huduma ya ardhi kwa wakati kwa wananchi, huduma ya utoaji wa Hatimiliki za
ardhi sasa ni kwenye kanda ambazo zinasimamiwa na Makamishna wa Ardhi Wasaidizi.”
Alisema Lukuvi.
Kanda
hizo ni kanda ya Dar es salaam inayojumuisha Manispaa za Ilala, Temeke na Kinondoni,
kanda ya Mashariki ambapo makao makuu yake yapo Morogoro, kanda ya Magharibi makao
yake makuu yapo Tabora, kanda ya Ziwa makao
yake makuu yapo Mwanza na kanda ya Kaskazini makao yake makuu yapo Moshi mkoani
Kilimanjaro.
Kanda
nyingine ni pamoja na kanda ya kusini ambayo makao yake makuu yapo Mtwara, kanda ya Kusini Magharibi makao yake makuu yapo
Mbeya na Kanda ya Kati ambayo makao yake makuu yapo mkoani Dodoma.
Katika kutoa
huduma yenye ubora kwa wananchi kwa wakati, Serikali kwa kushirikiana na Halmashauri
wataongeza watumishi wakada za wapimaardhi, wapangaji wa miji na vijiji pamoja na
wathaminia mbao watafanyakazi kwa pamoja kwenye kanda husika ambapo huduma ya ardhi
itakuwa karibu zaidi na wananchi.
Naye Balozi
wa Ireland nchini Tanzania Bi Fionnuala Gilsenan amempongeza Waziri Lukuvi na watendaji
wote wa wizara hiyo kwa kuwa mstari wa mbele katika kutoa huduma haraka na kwa wepesi
zaidi kwa jamii hatua ambayo ni yakupongezwa na kila mpenda maendeleo.
Balozi
Bi Gilsenan alisema kuwa ardhi nibidhaa muhimu inayoweza kutumika kwa kutoa huduma
mbalimbali za kijamii ikiwemo elimu, maji, barabara, ujenzi wa viwanda na miundo
mbinu mingine ili kumfanya mwananchi kupata huduma yenye tija kwa wakati.
Aidha,
kwa upande wake Kamishna wa Ardhi nchini Dkt. Moses Kusiluka alisema kuwa utoaji
wa huduma ya usimamizi wa ardhi umeanza kuboreshwa kwa kubadili mfumo wa utoaji
wa huduma kuwa wa kielekroniki kutoka mfumo wa kawaida, yaani‘manual’.
Dkt.
Kusiluka amesisitiza kuwa mfumo wa kielektroniki utaboresha sana utoaji wa huduma
za ardhi, ikiwa ni pamoja nak uondoa tatizo la milkipandikizi (double
allocation), kuondoa udanganyifu, kuongeza ufanisi wa watendaji na kuongeza mapato
ya Serikali.
Comments