WAZIRI WA FEDHA SAADA M.SALUM AFANYA UKAGUZI WA MATUMIZI WA MASHINE ZA EFD KATIKA MADUKA MKOANI DODOMA.
Mh.Waziri wa Fedha Saada Mkuya
Salum(MB) akitoa maelekezo kwa Meneja wa TRA mkoani Dodoma (mwenye
miwani) na wakala wa TRA kutoka Yono Action Mart kulifunga duka la
Salome Furniture baada ya kukutwa akifanya biashara bila ya kutumia
risiti za mashine ya EFD.
Mh.Waziri wa Fedha Saada
M.Salum(MB) akimsikiliza msimamizi wa duka la Salome Furniture wakati
akijitetea baada ya kukutwa anafanya biashara bila ya kutumia mashine ya
EFD.
Waziri wa Fedha Mh.Saada
M.Salum(MB) akiwa katika mgahawa wa Dodoma Carnival alipotembelea
kukagua matumizi ya mashine za EFD. Mh.Waziri aliagiza mgahawa huo
ufungwe mpaka hapo watakaponunua mashine hizo. Kushoto kwa Mh.Waziri ni
meneja wa TRA Mkoa wa Dodoma na mwenye shati jekundu ni msimamizi wa
mgahawa huo.
Waziri wa Fedha Mh.Saada Mkuya
Salum (MB) akiwa na Mh.Rukia Kassim Ahmed Mbunge wa viti maalum kupitia
chama cha wananchi CUF wakitoka kwenye duka ambalo lilikutwa mmiliki
wake akifanya biashara bila ya kutoa risiti za mashine ya EFD. (Picha
zote na Ramadhani Omary)
Mh.Waziri wa Fedha Saada Mkuya
Salum (MB) akijadiliana jambo na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano
Serikalini na Msemaji Mkuu wa Wizara ya Fedha Bi.Ingiahedi Mduma mara
baada ya kufanya ukaguzi wa matumizi ya mashine za EFD katika duka
mojawapo Mkoani Dodoma.
……………………………………….
Mh.Waziri wa Fedha Saada Mkuya Salum amefanya ukaguzi wa ghafla katika baadhi ya maduka Mkoani Dodoma ili kuona kama maelekezo ya Serikali kuhusu matumizi ya mashine za EFD yanatekelezwa ipasavyo.
Mh.Waziri wa Fedha Saada Mkuya Salum amefanya ukaguzi wa ghafla katika baadhi ya maduka Mkoani Dodoma ili kuona kama maelekezo ya Serikali kuhusu matumizi ya mashine za EFD yanatekelezwa ipasavyo.
Katika ukaguzi huo ambao
ulihusisha maduka ya kuuza thamani za majumbani,nguo na maduka ya kuuza
bidhaa mchanganyiko (Min supermarket),Mh.Waziri akiongozana na Watumishi
wa Mamlaka ya Mapato Tanzania aliagiza kufungwa kwa maduka yote ambayo
yamekaidi agizo la Serikali la matumizi ya mashine EFD mpaka pale
watakaponunua na kuzitumia ipasavyo mashine hizo.
Aidha Mh.Waziri amewataka
wafanyabiashara na wananchi kwa ujumla kuisaidia Serikali kuwafichua
wafanyabiashara wasio waaminifu na ambao wanapelekea kuikosesha Serikali
mapato ambayo yangetumika katika kuboresha huduma za kijamii.
Imetolewa na Msemaji Mkuu,
Wizara ya Fedha
Dodoma
Wizara ya Fedha
Dodoma
Comments