ZIARA YA RAIS WA ZANZIBAR Dk.Ali Mohamed Shein Nchini Ujerumani


????????????????????????????????????
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari wa Gazeti la Main Post la Mjini Wurzburg Nchini Ujerumani baada ya kulitembelea jingo la Serikali linalotumika kwa kwa shuhuli mbali mbali ikiwemo shuhuli za Utalii rais na ujumbe wake alitembelea jengo hilo akiwa katika ziara ya kikazi.
[Picha zote na Ramadhan Othman,
????????????????????????????????????
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein na Mkewe Mama Mwanamwema Shein wakipata maelezo kutoka kwa Mario Gerth (kulia) wakati waalipotembelea katika kituo cha maonesho ya picha Spitale katika Mji wa Wurzburg picha hizo zenye kuonesha Zanzibar na Ustaarabu wa Waswahili zilizotayarishwa chini ya nusimamizi wa Dr.Stefan Oschman Mkurugenzi wa Tamasha la Muziki wa Afrika.
????????????????????????????????????
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana  na Mratibu na Msimamizi Mkuu wa Mradi wa Zanzibar Amber Resort Bi Naila Jidawi wakati alipotembelea mabanda ya maonesho ya Kazi na sanaa za Mzanzibar katika viwanja vya maonesho katika Mji wa Wurzburg Nchini Ujerumani akiwa katika ziara ya kikazi nchini humo juzi.
????????????????????????????????????
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein na Mkewe Mama Mwanamwema Shein wakipata maelezo kutoka kwa  na Naibu   Katibu Mkuu Wizara ya Habari,Utamaduni,Utalii na Michezo Nd,Issa Mlingoti  wakati alipotembelea  mabanda ya maonesho ya Kazi na sanaa za Mzanzibar katika viwanja vya maonesho 27 ya Muziki wa Afrika  katika Mji wa Wurzburg Nchini Ujerumani akiwa katika ziara ya kikazi nchini na ujumbe nwake  juzi.
????????????????????????????????????
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein na Mkewe Mama Mwanamwema Shein wakiangalia picha za ramani ya ujenzi wa Mradi wa Zanzibar Amber Resort Bi Naila Jidawi wakati alipotembelea mabanda ya maonesho ya Kazi na sanaa za Mzanzibar katika viwanja vya maonesho katika Mji wa Wurzburg Nchini Ujerumani akiwa katika ziara ya kikazi nchini humo juzi.
????????????????????????????????????
Katibu Mtendaji wa Kamisheni ya Utalii Zanzibar Nd,Saleh Ramadhan Feruzi alipokuwa akitoa maelezo kwa wageni wakitalii mbali mbalio waliofika katika mabanda ya kazi mbali mbali kutoka Zanzibar wakati wa Maonesho ya Tamasha la 27 ya Muziki wa Afrika yaliyomalizika juzi katika viwanja vya Wurzburg Nchini Ujerumani ambapo mgeni rasmi alikuwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein alipofanya ziara ya kikazi ya siku nane nchini humo,
????????????????????????????????????
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein na Mkewe Mama Mwanamwema Shein wakiangalia kazi mbali mbali za kiutamaduni wa Zanzibar ikiwemo kusuka ukili,mikoba na utiaji wa hina na wanja kwa watalii waliotembelea  mabanda ya maonesho ya Kazi hizo katika viwanja vya maonesho katika Mji wa Wurzburg Nchini Ujerumani akiwa katika ziara ya kikazi nchini humo juzi.
????????????????????????????????????
Mchoraji wa mauwa kutumia wanja na hina akiwaremba watalii wakati wa maonesho ya 27 ya Tamasha la muziki wa Taarab kutoka Zanzibar pia Tamasha lilijumuisha wasanii mbali mbali wa fani hiyo kutoka nchi mbali mbali Duniani na kazi za kiutamaduni katika kuitangaza Zanzibar Kiutalii katika Mji wa Wurzburg Nchini Ujerumani juzi,
????????????????????????????????????
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) na Mkewe Mama Mwanamwema Shein (kulia)  wakipata maelezo kutoka kwa Katibu Mtendaji wa Kamisheni ya Utalii Zanzibar Nd,Saleh Ramadhan Feruzi walipoangalia kazi mbali mbali za uchoraji ikiwa ni katika hatua za kukuza Utalii wa Zanzibar katika   mabanda ya maonesho ya Kazi hizo katika viwanja vya maonesho katika Mji wa Wurzburg Nchini Ujerumani akiwa katika ziara ya kikazi nchini humo juzi.
????????????????????????????????????
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein na Mkewe Mama Mwanamwema Shein (kushoto)  wakipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi Masoko Salum A.Kibe wakati  walipoangalia bidhaa  mbali mbali za karafuu  ikiwa ni katika hatua za kukuza Utalii wa Zanzibar katika   mabanda ya maonesho   katika Mji wa Wurzburg Nchini Ujerumani juzi akiwa katika ziara ya kikazi.
????????????????????????????????????
 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein alipokuwa akibadilishana mawazo na Viongozi wa baada ya kutembelea sehemu mbali mbali za maonesho ya Tamasha la 27 la  Muziki ambapo Zanzibar ilishiriki   kujitangaza kiutalii na kuonesha bidhaa mbali mbali katika maonesho hayo yaliyofanyika katika viwanja vya Eneo maalum lililotengwa Mjini Wurzburg Nchini Ujerumani katika ziara ya kiazi ya siku nane nchini humo,
????????????????????????????????????
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein na ujumbe wake walipofika katika viwanja vya maonesho na kuwatembelea wasanii wa kikundi cha muziki wa Taarab cha Matona kutoka Zanzibar na kuwapa moyo katika jitihada zao za kuitangaza Zanzibar Kiutalii Nchini Ujerumani katika Tamasha  27 la  Muziki  katika ziara ya kiazi ya siku nane nchini humo,
????????????????????????????????????
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein na Mkewe Mama Mwanamwema Shein wakifuatana na Dr.Stefan Oschman Mkurugenzi wa Tamasha la Muziki wa Afrika baada ya kutembelea mabanda ya maonesho ya Zanzibar katika Mji wa Wurzburg  Nchini Ujerumani katika hatua zakuitangaza Zanzibar kiutalii.
????????????????????????????????????
????????????????????????????????????Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akiagana na Mkuu wa Idara ya magonjwa ya Tropiki  Prof.Dr.med.Augustin Stich baada ya Taasisi ya Tafiti mbali mbali yakiwemo magonjwa ya Binadamu, Chuo cha Afya katika Mji wa Wurzburg kimeweza kutoa mchango mkubwa katikakupambana na maradhi ya Ebola yaliyotokea Nchi za Magharibi,

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.