Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul
Makonda (katikati) akikata utepe kuzindua rasmi tawi la benki ya First
National la Mbezi Beach jana jijini Dar es salaam huku akiambatana na
Balozi wa Heshima wa Djibouti Said Shamo na Mkuu wa Huduma za Rejareja
wa benki hiyo, Francois Botha.
Mkuu wa Bidhaa na Huduma za
Mitandao, Silvest Arumasi akimpa maelekezo Mkuu wa wilaya ya Kinondoni,
Paul Makonda mara baada ya kufungua rasmi tawi la benki ya First
National la Mbezi Beach jana jijini Dar es salaam. Pembeni yake ni
Balozi wa Heshima wa Djibouti Said Shamo.
Mkuu
wa Huduma za Rejareja wa benki hiyo, Francois Botha akiongea machache
wakati wa ufunguzi rasmi tawi la benki ya First National la Mbezi Beach
jana jijini Dar es salaam.
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda akitoa shukrani zake za pekee
kwa benki ya First National kwa kuendelea kufungua matawi yake pembezoni
mwa mji wa Dar es Salaam ambapo alisema ni jambo la faraja sana pale
mteja anapofuatwa alipo na si kila siku kukimbilia kufungua benki
katikati ya mji.
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda (wa pili toka kulia) akiwa na Balozi wa Heshima wa Djibouti Said Shamo ( kwanza kulia) pamoja na viongozi wa benki ya First National. Kulia ni Mkuu wa Huduma za Rejareja, Francois Botha na Mkuu wa Bidhaa na Huduma za Mitandao, Silvest Arumasi.
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda akiongea machache na mmoja ya kiongozi wa Benki hiyo.
Comments