JK ASIFIA SEKTA BINAFSI KUKUBALI KUSAINI MKATABA UADILIFU

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amesema kuwa uamuzi wa Sekta Binafsi kukubali kubanwa na sheria, taratibu na maadili ya kukabiliana na rushwa ni hatua kubwa ya kubadilisha mapambano (Game Changer) dhidi ya rushwa nchini.

“Hapa sasa tunaongeza utamu kwenye keki (icing on the cake) kwa sababu hii ni mara ya kwanza katika historia ya nchi yetu kwa sekta binafsi kukubali kubanwa na maadili ya mapambano dhidi ya rushwa,” Rais Kikwete amesema leo, Ijumaa, Agosti 14,2015 wakati alipozungumza katika Halfa ya Uzinduzi wa Ahadi ya Uadilifu.

Katika hafla hiyo iliyofanyika Ikulu, Dar es Salaam, Rais Kikwete amekuwa kiongozi wa kwanza nchini kutia saini Hatia ya Ahadi ya Uadilifu ambayo itatiwa saini na viongozi wote wa umma, watumishi wote wa umma na viongozi wa sekta binafsi nchini ikiwa ni hatua nyingine za kuzidi kupambana na rushwa na kuboresha utawala bora nchini.

Rais Kikwete amewaambia viongozi waliohudhuria hafla hiyo kuwa viongozi wa umma nchini wamekuwa na miiko, tarartibu na kanuni mbali mbali ambazo zimekuwa zinawabana na kuongoza maadili yao tokea uhuru wa Tanzania. “Hawa wamekuwa na nyaraka nyingi ambazo zimekuwa zinawabana tokea uhuru wa nchi yetu. Lakini sekta binafsi haijapata kuwa na miiko ya namna hii.”

Rais Kikwete ameongeza kusema kuwa hiyo ilikuwa mara ya kwanza kwa sekta binafsi kukubali kubanwa na miiko ya uongozi na katika hafla ya leo, Sekta Binafsi imewakilishwa na Mwenyekiti wa Watendaji Wakuu wa Makampuni nchini, Ndugu Ali Mufuruki ambaye pia ni Mwenyekiti na Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Infotech Investments.

Ndugu Mufuruki pia ametia saini Hati ya Ahadi ya Uadilifu kwa niaba ya Sekta Binafsi nchini.

Rais Kikwete pia ametoa changamoto kwa sekta binafsi, akiwataka watendaji wa sekta hiyo kujitokeza na kutoa habari kuhusu rushwa kwa sababu kwa kuwa baadhi ya watendaji na watumishi wa sekta bianafsi ni washiriki katika rushwa kwa maana ya kuwarubuni watumishi wa umma na viongozi wa sekta ya umma.

Amesema kuwa ni jambo lisilokuwa na manufaa kwa watendaji wa sekta binafsi kukaa tu na kulalamika kuwa kuna rushwa nchini wakati wao pia ni washiriki.

“Jitokezeni waziwazi na kutupa habari ya watu ambao wanawadai rushwa walioko katika sekta ya umma. Kujitolea habari za namna hii kutasaidia. Na katika hili mtu haihitaji wala kushindwa na sharia yoyote. Ni wajibu wake kama raia bora.

Ahadi ya Uadilifu ni moja ya hatua ambazo zilipendekezwa na wadau katika moja ya warsha za kujadili jinsi gani ya kukabiliana na balaa la rushwa nchini chini ya Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN) ambao ulianzishwa na Serikali ya Rais Kikwete.

Wadau hao walitoa pendekezo hilo kwa Serikali kama moja ya njia za kuzidi kukabilaiana na rushwa nchini.

Ends


Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.