Baadhi
ya wafanyakazi wa mfuko wa bima ya afya NHIF kigoma wakikabidhi msaada
wa vyakula kwa uongozi wa kituo cha Silabu cha kulelea wazee wasiojiweza
ikiwa leo ni siku ya maadhimisho ya siku ya wazee duniani.
Meneja wa Mfuko wa bima NHIF ya kigoma akisalimiana na wazee wanaotunzwa katika kambi ya Silabu kata ya kibirizi
Baadhi ya wazee wasiojiweza wanaoishi na kutunzwa katika kambi ya kulea wazee ya Silabu kata ya Kibirizi Mkoani hapa.
Na Editha Karlo.Kigoma
MFUKO
wa Bima ya afya (NHIF)wametoa msaada wa vyakula kwa wazee wasiojiweza
uliopo katika kituo cha silabu kata ya kibirizi mjini hapa.
Akiongea
baada ya kukabidhi msaada huo wa chakula Meneja wa Mkoa wa mfuko huo
Elius Odhiambo alisema kuwa mfuko unatumbua umuhimu na mchango wa wazee
kwa jamii.
"Sisi
kama mfuko wa bima ya afya tuna thamini sana na kutambua mchango wenu
wazee kwa jamii kwani kila mmoja wetu ni mzee mtarajiwa"alisema odhiambo
Alisema
wamekabidhi msaada wa chakula wenye thamani ya shilingi milioni moja na
elfu sitini,vyakula walivyotoa ni mchele kilo 100,sukari kilo 100,unga
wa ugali kilo 100,maharage kilo 100 na mafuta ya kupikia kilo 20
Meneja huyo alisema wataendelea kusaidiana na kuwasaidia wazee hao kila inapobidi.
Naye
mkuu wa kituo hicho cha kutunzia wazee Juma Ndikamukana wasiojiweza
aliushukuru mfuko wa bima ya afya kwa msaada wao huo na kuwakumbuka
wazee katika siku yao leo.
Alisema kituo hicho kina jumla ya wazee 51 wasiojiweza wanaotunzwa wanaotoka maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Kigoma
Comments