MKUU WA WILAYA YA SHINYANGA AFANYA MKUTANO NA AKINA MAMA ZAIDI YA 300 KUPAMBA NA KIPINDUPINDU SHINYANGA




Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro akizungumza wakati wa mkutano wake na wanawake zaidi ya 300 katika manispaa ya Shinyanga uliofanyika katika ukumbi wa NSSF mjini Shinyanga ambapo pamoja na mambo mengine alisema wanawake ni jeshi kubwa na ni walimu wakubwa katika familia hivyo wana nafasi kubwa ya kupambana na kipindu pindu kwa kuimarisha na kuhamasisha usafi kwa akina baba,watoto na hata wanawake wenzao.
"Kipindu pindu ni hatari sana...kinaua lazima tupambane nao kwa nguvu zote..nimewaita ili kila mmoja ajue Shinyanga tuna janga..sasa kila mtu achukue hatua,ugonjwa huu unatokana na uchafu..akina mama mna nafasi kubwa sana katika hili...."alisema Matiro.
Akina mama wakiwa wamenyoosha mikono...kwamba wako tayari kupambana na kipindupindu.

Hapa ni katika ukumbi wa NSSF mjini Shinyanga ambako wanawake/akina mama zaidi ya 300 wa manispaa ya Shinyanga wamekutana kujadili namna ya kupambana na ugonjwa wa Kipindupindu ambao umeukumba mkoa wa Shinyanga.Mkutano huo umeitishwa na mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro.Akina mama hao waliojitokeza kwa wingi leo jioni Oktoba 06,2015 wameweka mikakati mbalimbali ya kutokemeza ugonjwa kipindupindu ambapo Jana pekee wagonjwa 9 wamelazwa katika kambi maalum jirani na hospital ya rufaa ya mkoa wa Shinyanga ambapo kati ya hao 9 wawili wamefariki dunia.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.