Ndege
ya kijeshi ya Marekani aina ya C-130 Hercules imeanguka usiku wa leo
katika Uwanja wa Ndege wa Jalalabad nchini Afghanistan na kuua watu 12.
Kanali
wa jeshi la Marekani Brian Tribus ameiambia AFP kwamba watao kati ya
waliokufa walikuwa wanajeshi wa Marekani, watano walikuwa raia wa
kawaida na wawili walikuwa ni Waafghan.
Msemaji
wa kundi la wapiganaji la Taliban, Zabihullah Mujahid alisema kupitia
Twitter kwamba kundi hilo lilitungua ndege hiyo, lakini mashirika ya
habari yanasema hakuna ishara inayoonesha ndege hiyo kama ilishambuliwa.
Jeshi la Marekani limesema linachunguza kilichosababisha ajali hiyo.
Ajali
hiyo ya ndege imetokea huku ndege za kijeshi za Marekani zikisaidiana na
wanajeshi wa Afghanistan kujaribu kukomboa mji wa Kunduz uliotekwa na
wapiganaji wa Taliban.
Takriban
wanajeshi 10,000 wa Marekani wamo Afghanistan baada ya mpango wa
kuondoa majeshi hayo asteaste kubadilishwa mapema mwaka huu.
Rais
Obama alikuwa ameahidi kuacha wanajeshi wachache sana wa Marekani nchini
humo ambao wangekuwa wa kulinda ubalozi wa Marekani kufikia mwisho wa
mwaka 2016.
Comments