RAIS JAKAYA KIKWETE AKIWA NA RAIS BARACK OBAMA


post-feature-image
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na   Mhe.Barack Obama na Mkewe  Michelle  Obama wakati wa hafla  ilioandaliwa na  Rais wa Marekani kwaajii ya   Viongozi wa Wakuu  Nchi na Serikali wanaohudhuria Mkutano wa 70 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa ( Picha hii ni kwa hisani ya  Ofisi ya Itifaki ya White House)
Mhe. Rais Kikwete akiwa na  Mhe. Sophia Simba, Katibu Mkuu  Balozi  Liberata Mulamula na mwanamitindo  Flaviana Matata muda mfupi mara baada ya kulihutubia  Baraza Kuu la  70 la Umoja wa Mataifa
Mwakilishi wa Kudumu wa  Antigua na Bermuda  Balozi  Walton Alfonso Webson ambaye ni  mlemavu wa kutoona   akimwongoza Mhe. Rais Kikwete kwenda kuonana na   Waziri Mkuu wake, Mhe. Gaston Alphoso Browne aliyekuwa na mazungumzo wa Mhe.Rais mara baada ya Mhe. Rais kulihutubia  Baraza  Kuu la 70 la Umoja wa Mataifa.
Mhe. Rais Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika mazungumzo na  Waziri Mkuu wa Antigua na Barbuda Mhe. Gaston Alphonso Browne,  wengine katika mazungumzo hayo ni Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa,  Balozi Tuvako  Manongi,  Mwakilishi wa kudumu wa Antigua na Barbuda, Balozi Walton  Webson mwenye miwani myeusi na Mkurungezi wa  Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa Balozi  Celestin Mushy
--
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete jana jumanne amelihutubia kwa mara ya mwisho Baraza Kuu la 70 la Umoja wa Mtaifa akiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. 

 Hotuba ya Mhe. Rais na ambayo iligusia mambo mengi ya kisiasa, kiuchumi, na maendeleo akitumia pia fursa hiyo kuwaanga viongozi wenzie na kuwashukuru kwa ushirikiano waliompatia katika kipindi cha miaka kumi ya uongozi wake, iliwasisimua wajumbe wa mkutano huo kiasi cha kukatishwa mara kwa mara kwa makofi. 

 Zifuatazo ni baadhi ya picha zinazomwonyesha Mhe. Rais katika Matukio mbalimbali Moja wapo likiwa ni hafla ambayo Rais wa Marekani, Mhe Barack Obama aliiandaa kwaajili wa Viongozi Wakuu wa Nchi na Serikali waliohudhuria Mkutano wa 70 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa. Picha kwa hisani ya Uwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.