ZANTEL YATEMBELEA CHAMA CHA MAALBINO TANZANIA

 Mmoja wa wafanyakazi wa Chama Cha Albino, Christina Mbedi akielezea namna Chama cha Albino kinavyofanya kazi zake kwa Meneja wa Chapa na Mawasiliano wa Zantel, Arnold Madale wakati wa ziara ya viongozi wa Zantel ofisini kwao. Anayetizama kulia ni Mwenyekiti wa Chama cha Umoja wa Albino Tanzania, Ernest Kimaya.
Meneja wa Chapa na Mawasiliano wa Zantel, Arnold Madale akikabidhi msaada wa vifaa vya mawasiliano kwa Mwenyekiti wa Umoja wa Chama cha Albino Tanzabua, Ernest Kimaya. Wanaotazama nyuma ni baadhi ya viongozi wa Chama cha Albino.
 Meneja wa Chapa na Mawasiliano wa Zantel, Arnold Madale akikabidhi msaada wa vifaa vya mawasiliano kwa Mwenyekiti wa Umoja wa Chama cha Albino Tanzania, Ernest Kimaya. Anayetazama nyuma ni mmoja wa viongozi wa Chama cha Albino.
Viongozi wa Chama cha Albino na Zantel wakiwa katika picha ya pamoja baada ya Viongozi wa Zantel kutembelea ofisi zao.


  • Yaiunganisha ofisi ya chama cha albino na huduma ya mtandao pamoja na mawasiliano ya simu
Dar es Salaam, 8/10/2015: Uongozi wa Kampuni ya simu za mikononi ya Zantel leo umetembelea ofisi za Chama cha Maalbino Tanzania, ziara yenye lengo la kujifunza zaidi kuhusu Chama cha Maalbino kinavyofanya kazi pamoja na kuboresha ushirikiano baina yao.
Pamoja na kuzungumza na viongozi wa chama cha Maalbino, uongozi wa Zantel pia umekabidhi huduma za simu, kwa kuwapa namba maalumu pamoja na kuwaunganisha na huduma ya mtandao.
Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Mkurugenzi wa Masoko wa Zantel, Progress Chissenga alisema huu ni mwendelezo wa ushirikiano baina ya Zantel na Chama Cha Maalbino.
‘Leo tumeamua kuja kuwatembelea wenzetu wa Chama cha Maalbino ili kujionea namna wanavyofanya kazi, na msaada huu wa intaneti pamoja na huduma ya simu tuliyokabidhi leo itawawezesha viongozi na watendaji wa chama cha albino kupiga simu bure kwa mwaka mzima, lakini pia itarahisisha mawasiliano baina yao na viongozi wengine wa chama kutoka mikoani’ alisema Chissenga.
Katika ziara hiyo, viongozi wa Zantel na Chama cha Maalbino Tanzania walijadiliana maeneo mengine ya kuongeza ushirikiano baina yao katika kuhakikisha chama cha Maalbino kinatekeleza majukumu yake zaidi.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Albino Tanzania, Bwana Ernest Kimaya, alisema wanaishukuru kampuni ya Zantel kwa kuendelea kuwaunga mkono katika juhudi zao za kuhakikisha mauaji ya albino yanamalizika nchini.
‘Tunawashukuru Zantel kwa kuendelea kutuunga mkono na msaada huu waliotukabidhi leo, unaonyesha kuwa wana nia ya dhati ya kushirikiana na chama chetu’ alisema Kimaya.
Ziara hii ni mwendelezo wa ushirikiano baina ya Kampuni ya simu za mikononi ya Zantel na Chama cha Maalbino Tanzania, ambao ulilenga kusambaza elimu juu ya ulemavu.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA

DKT NCHIMBI ASHIRIKI MAZISHI YA ASKOFU.GACHUMA WA KANISA LA NLGCC

π™‚π˜Όπ™ˆπ™Šπ™‰π˜Ώπ™„ π™†π˜Όπ˜Ύπ™ƒπ™€π™•π˜Ό π™†π™„π˜½π™„π™‰π™‚π™’π˜Ό.