Arsenal dhidi ya Leicester, Man City na Tottenham


LeicesterImage copyrightReuters
Image captionLeicester kwa sasa wanaongoza ligini
Mechi zitakazochezwa Jumapili baina ya timu 4 za kwanza zitaamua mwelekeo halisi wa ligi hii yenye wapenzi wengi duniani, Ligi Kuu ya Uingereza.
Arsenal itamenyana na Leicester City ambayo bado inaongoza ligi ikiizidi Arsenal alama 5.
Arsenal imo kwenye nafasi ya tatu na ushindi wake utapunguza pengo baina yake na Leicester na kuipa matumaini zaidi ya kuendelea kupigana hadi mwisho.
Nayo Manchester City yenye nafasi ya 4 itaialika Tottenham iliyo kwenye nafasi ya pili.
Bila shaka mshindi atajiweka katika nafasi nzuri ya kuendelea na mbio za kuwania ubingwa.
Miongoni mwa mechi zitakazopigwa jumamosi hii ni Sunderland kupepetana na Manchester United na Everton kuzipiga na West Brom.
Ratiba kamili na kama ifuatavyo (Saa za Afrika Mashariki

Jumamosi tarehe 13 Februari:

  • Sunderland v Man Utd 15:45
  • Bournemouth v Stoke 18:00
  • Crystal Palace v Watford 18:00
  • Everton v West Brom 18:00
  • Norwich v West Ham 18:00
  • Swansea v Southampton 18:00
  • Chelsea v Newcastle 20:30

Jumapili tarehe 14 Februari

  • Arsenal v Leicester 15:00
  • Aston Villa v Liverpool 17:05
  • Man City v Tottenham 19:15

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

NI SIMBA PEKEE ILIYOFUNGWA ROBO FAINALI

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KINANA ASIMIKWA KUWA MMOJA WA MACHIFU WA WAPARE, SAME MAGHARIBI

DK NCHIMBI AMTEMBELEA MZEE YUSUF MAKAMBA*

AZIZ KI AAHIDI KILA ATAKAYEIFUNGA MAMELODI

HATUTOPAKI BASI DHIDI YA YANGA-MOKWENA

“PEMBA SALUTI KWENU” DK. NCHIMBI*

DKT NCHIMBI AWAAHIDI MAKUBWA WANANCHI WA KWELA, RUKWA