YANGA SC YASHINDA 1-0 MAURITIUS, MAMBO YA NGOMA HAYO!


Na Princes Akbar, CUREPIPE
BAO pekee la mshambuliaji Mzimbabwe, Donald Ngoma limeipa mwanzo mzuri Yanga SC katika mchezo wa kwanza Raundi ya Awali Ligi ya Mabingwa Afrika, baada ya kuwafunga wenyeji Cercle de Joachim 1-0 mchana wa leo Uwanja wa Curepipe mjini Curepipe, Mauritius.
Kwa ushindi huo, Yanga SC sasa watakuwa na kazi nyepesi katika mchezo wa marudiano wiki mbili zijazo mjini Dar es Salaam, wakihitaji hata sare ili kusonga mbele, ambako watakutana na mshindi kati ya APR ya Rwanda na Mbabane Swallows ya Swaziland.
Katika mchezo huo uliochezeshwa na marefa wa Madagascar, Hubert Marie Bruno Andriamiharisoa, Randrianarivelo Ravonirina Harizo na Augustin Gabriel Herinirina, Ngoma alifunga bao hilo dakika ya 17 tu akimalizia krosi maridadi ya beki wa kulia, Juma Abdul Jaffar. 
Kikosi cha Yanga SC kilichoilaza 1-0 Cercle de Joachim leo

Yanga SC ilipata pigo kipindi cha pili, baada ya mpishi wa bao lake, Juma Abdul Jaffar kuumia na kushindwa kuendelea na mchezo, nafasi yake ikichukuliwa na Pato Ngonyani, aliyemalizia vizuri. 
Baada ya mchezo huo, Yanga SC inatarajiwa kupanda ndege ya ATC waliyokwenda nayo huko, kuelekea kisiwani Pemba kuweka kambi ya kujiandaa na mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara dhidi ya mahasimu, Simba SC Jumamosi wiki ijayo Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Kikosi cha Yanga kilikuwa; Ally Mustafa 'Barthez', Juma Abdul/Pato Ngonyani dk70, Oscar Joshua, Kevin Yondan, Vincent Bossou, Thabani Kamusoko, Simon Msuva, Haruna Niyonzima, Donald Ngoma, Amissi Tambwe/Paul Nonga dk68 na Deus Kaseke.
Kikosi kamili cha Yanga kinachokwenda kambini Pemba ni makipa; Ally Mustafa ‘Barthez’, Deo Munishi ‘Dida’ na Benedicto Tinocco.
Mabeki; Juma Abdul, Mbuyu Twite (DRC), Oscar Joshua, Mwinyi Hajji Mngwali, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Kevin Yondan, Vincent Bossou (Togo) na Pato Ngonyani.
Viungo ni; Said Juma ‘Makapu’, Salum Telela, Thabani Kamusoko (Zimbabwe), Haruna Niyonzima (Rwanda), Simon Msuva, Issoufou Boubacar (Niger), Godfrey Mwashiuya na Deus Kaseke.
Washambuliaji ni; Malimi Busungu, Paul Nonga, Amissi Tambwe (Burundi) na Donald Ngoma (Zimbabwe).
BENCHI LA UFUNDI; Kocha Mkuu; Hans van der Pluijm (Uholanzi), Kocha Msaidizi; Juma Mwambusi, Kocha wa Makipa; Juma Pondamali
Daktari; Nassor Matuzya, Meneja; Hafidh Saleh, Mchua Misuli; Jacob Onyango na Mtunza Vifaa; Mohammed Mpogolo.

Comments

HABARI ZILIZOSOMWA ZAIDI

MAKABILA 10 YENYE WANAWAKE WAREMBO TANZANIA

HAKUNA BINADAMU ALIYESALIMIKA NA UPOFU HUU...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA WATANZANIA WATAKAOVAA JEZI ZA MAMELODI AU AL AHLY

CHATANDA AFUNGUA MAFUNZO YA KUWAJENGEA UWEZO MADIWANI WANAWAKE WA MIKOA 11

KOCHA BENCHIKHA AMESEPA

MASHUSHUSHU WA MAMELODI WALIKUJA KUTUPELELEZA: HERSI

KOCHA WA AL.AHLY ASEMA YANGA NI TIMU BORA NA NGUMU