Askari wa Bunge wakimtoa nje ya Bunge Mbunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki, Joshua Nassari baada ya kuonekana kuhamasisha wabunge wa Kambi ya Upinzani kufanya vurugu baada ya muongozo wake wa kutaka kujadiliwa kwa hoja ya serikali kuwatimua wanafunzi 7802 wa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) bungeni Dodoma leo.
Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako akitoa tamko la serikali kuhusu kufukuzwa kwa wanafunzi wa Udom, jambo ambalo lilisababisha vurugu na Bunge kuahirishwa kwa muda.
Mbunge wa Jimbo la Chemba, Juma Mkamia akiomba muongozo kwa Naibu Spika akitaka suala la kufukuzwa wanafunzi lijadiliwe bungeni.
Wabunge wa Kambi ya Upinzani wakiwa wamesimama kuunga hoja iliyotolewa na Mkamia
Wabunge wa CCM wakiwa wamesimama kuunga mkono muongozo uliotolewa na Mkamia
Naibu Spika, Dk. Tulia Ackson akiwasihi wabunge kuacha kufanya vurugu
Nassari akiomba muongozo akitaka suala la kutimuliwa kwa wanafunzi wa Udom lijadiliwe bungeni
Wabunge wakitolewa bungeni baada vurugu kutokea
Mtafaruku bungeni
Mbunge wa Mlimba Suzan Kiwanga akilalamika baada ya Bunge kuahirishwa
Wabunge wakitoka baada ya Bunge kuahirishwa
Comments