Chama Cha Wananchi (CUF) kimewasimamisha uanachama aliyekuwa Mwenyekiti wa chama hicho, Profesa Ibrahim Lipumba
Aliyekuwa
Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho upande wa Bara, Magdalena
Sakaya,ambaye pia ni Mbunge wa jimbo la Kaliua Mkoani Tabora.
Uamuzi
huo umetolewa jana na Baraza Kuu la Chama hicho lililofanya mkutano
wake visiwani Zanzibar kwa lengo la kuwajadili wanachama kadhaa wakiwemo
vigogo hao. Sakaya amevuliwa nyadhifa zote ndani ya chama kabla ya
kusimamishwa.Taarifa kutoka ndani ya Mkutano huo zimeeleza kuwa Baraza
hilo limewaadhibu wanachama 15 wakiwemo Sakaya ambaye pia ni mbunge wa Kaliua.
Mbali
na vigogo hao, wengine waliopigwa rungu na Baraza Kuu la CUF ni pamoja
na Katibu wa Baraza la Wazee, Shashi Lugeye, Thomas Malima na Naibu
Mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano, Abdul Kambaya.Aidha, Baraza hilo
limemsimamisha uanachama Mbunge wa Mtwara Mjini, Maftah Nachuma. Hatua
hii inaweka matatani ubunge wa Sakaya na Nachuma kwani wakifikia hatua
ya kufukuzwa watakosa sifa za kuendelea kuwa wabunge.
Lipumba
na Sakaya hawakupata nafasi ya kujitetea kutokana na kutohudhuria
mkutano huo wakati Shashi alipata nafasi ya kujitetea kutokana na uwepo
wake lakini utetezi wake haukuzaa matunda. Katiba ya chama hicho haiwapi
nafasi wabunge hao kukata rufaa kutokana na uamuzi wa Baraza hilo.
Uamuzi
huo umekuja ikiwa ni siku chache baada ya Mkutano Mkuu Maalum wa Chama
hicho uliolenga kumchagua Mwenyekiti Mpya kuvunjika kutokana na kuwepo
vurugu kubwa baada ya Profesa Lipumba kuingia ndani ya ukumbi huo na
wafuasi wake wakitaka barua yake ya kutaka kurejea kwenye nafasi yake
ijadiliwe na kukubaliwa.
Hata
hivyo, kura zilizopigwa na wajumbe wote zaidi ya 800, ni kura 14 pekee
zilizotaka Profesa Lipumba aendelee na nafasi ya uenyekiti.
Kwa
mujibu wa taarifa zilizopatikana zimeeleza kuwa wanachama wapatao 11 na
majina yao haya hapa chini wamesimamishwa uanachama.
Wanachama hao ni :
1. Prof Ibrahim Lipumba
2. Magdalena Sakaya
3. Abdul Kambaya
4. Ashura Mustapha
5. Omar Mhina
6. Thomas Malima
7. Kapasha Kapasha
8. Maftaha Nachuma
9. Mohammed Habib Mnyaa
10. Haroub Shamis
11. Mussa Haji Foum
Comments