Gianluigi Buffon aliachwa kwenye benchi Juventus walipokuwa wanacheza dhidi ya Sampdoria, hatua ambayo huenda iliwagharimu Jumapili.
Walipokezwa kichapo cha 3-2.
Buffon aliwekwa kwenye benchi pamoja na beki Andrea Barzagli, kwa sababu wanahitaji "muda kusahau" masaibu ya kukosa kufuzu kwa Kombe la Dunia.
Massimiliano Allegri aliwapumzisha wawili hao, ambao tayari wamestaafu soka ya kimataifa, baada ya Italia kushindwa na Sweden mechi za muondoano wa kufuzu.
- Buffon achukua nafasi ya Neuer kikosi bora cha Fifa
- Buffon aomba msamaha kwa niaba ya Italia na kustaafu kimataifa
- Bao la Giroud lashinda tuzo ya Puskas
Sampdoria waliongoza kupitia bao la kichwa la Duvan Zapata, Lucas Torreira na Gianmarco Ferrari nao wakaongeza na kufanya mambo 3-0.
Gonzalo Higuain na nguvu mpya Paulo Dybala walikomboa mawili dakika za mwisho.
Juventus wamesalia alama nne nyuma ya viongozi wa ligi Napoli ambao bado hawajashindwa.
Inter Milan waliwapiku na kuingia nafasi ya pili baada ya kuwashinda Atalanta 2-0 baadaye Jumapili.
Goalkeeper Buffon, 39 - ambaye anahitaji mechi 21 kuweka rekodi mpya ya uchezaji mechi nyingi zaidi Serie A, anapanga kustaafu mwisho wa msimu Juve wasiposhinda Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya.
Comments